Kufanya
sensa ya kuwatambua watu wenye mahitaji maalumu kwa kupitia mamlaka za Serikali
za Mitaa, viongozi wa dini, viongozi wa kisiasa na viongozi wa kimila kwa kushirikisha
Jamii yenyewe kwa kutembelea nyumba hadi nyumba la Eneo husika.
1. kutoa Elimu kwa Jamii umuhimu wa Afya ya Mama
Mjamzito na Watoto wenye umri chini ya
miaka 5 kwa kushirikisha Jamii.
2. Kuwaunganisha watu mbalimbali, mashirika ya
ndani na nje katika kuwasaidia watoto wenye mahitaji maalum na wamama
wajawazito kuwasaidia kupata huduma za msingi kama vile; Afya, Elimu, Chakula,
Makazi na Mavazi
3. Kuhakikisha
upatikanaji wa vitendea kazi na vifaa vya kujifunzia na kufundishia kwa watoto
wenye mahitaji maalumu vinapatikana kwa kuishirikisha Jamii, watu binafsi,
pamoja na mashirika mbalimbali kutegemea na aina ya ulemavu alionao mtoto.
4. Kuhakikisha
shirika linakuwa na kituo chake cha Redio na TV kitakachosaidia katika
kuelimisha Jamii suala zima la umuhimu wa kuwahudumia watoto walemavu, wamama
wajawazito na watoto wenye umri chini ya miaka 5 pamoja na mazingira.

0 comments:
Post a Comment